Ebu Mfahamu Melissa Magiera, model kwenye video ya ‘Ntampata Wapi’

No comments
Diamond Platnumz amewapa mashabiki wake kile walichokuwa wakikingoja kwa muda mrefu, akaunti ya Instagram ya mrembo aliyemtumia kwenye video ya wimbo wake ‘Ntampata Wapi’. 


“Haya sasa, najua mlikuwa mkisubiria kwa mda mreeeeefu, hii ndio Instagram Aacount ya yule dada alonisaliti kwenye video ya #Ntampata_Wapi. .Basi nnavyowajua atatongozwa leo hadi akome, makuwadi sasa,” ameandika Diamond kwenye picha aliyoweka Instagram akiwa na msichana huyo.
010
Kwenye mahojiano na Bongo5 hivi karibuni, Diamond alisema alifurahishwa na jinsi msichana huyo alivyoigiza kwenye video yake.
“Kiukweli amejitahidi na amefanya vizuri sana. Bado tunawasiliana, hata juzi nilimtumia meseji nikamwambia ‘Melissa natamani ujue jinsi gani unazungumziwa, nikasema ‘najua kabisa huko South Africa hawawezi kuwa wanaizungumzia hii video kama wanavyoizungumzia hii video huku nyumbani, natamani ujue jinsi gani walivyokupokea, natamani ujue umefahamika kiasi gani. Nikamwambia ‘siku ntakutag Instagram, halafu utaona shughuli yake.’ Ntamuweka siku moja Instagram, najua watu wanasubiri akaunti yake,” alisema.
003
Msichana huyo anaitwa Melissa Magiera, na yupo chini ya kampuni ya Ice Model Management, tawi la Cape Town na ‘Ntampata Wapi’ ndio video yake ya muziki ya kwanza kuwahi kufanya.
Kupitia kupitia akaunti yake ya Facebook, October 15 alipost picha ya behind the scenes ya video hiyo na kuandika: 19 hour shoot! Featured in my first music video. Unfortunately I cannot show any other pictures.”
Tazama zaidi picha zake.
046
045
043
040
037
033
028
027
024
023
022
021017
016
055

No comments :

Post a Comment