Kuhusiana na kuvuja kwa picha za utupu za huyu staa wa muziki Uganda, Serikali imeingilia kati

No comments
DesireWaziri wa Maadili wa Uganda Simon Lokodo ameagiza kukamatwa kwa msanii Franklin kutoka Nigeria ambaye anatuhumiwa kwa kusambaza picha za utupu alizopiga akiwa na mpenzi wake Desire Luzinda.
Serikali ya Uganda ilipitisha sheria ya ‘Anti-ponography’ ambapo kusambaa kwa picha hizo kunamtia hatiani jamaa huyo kwa kuvunja sheria hiyo,iwapo atakutwa na hatia adhabu yake ni faini ya milioni 50 za Uganda sawa na dola elfu 20 ambazo ni zaidi ya milioni 30 za Kitanzania au kifungo cha miaka 10.
Franklin anatafutwa kwa kuvujisha picha hizo ambapo inasemekana kuvunjika kwa uhusiano wao kumepelekea jamaa huyo kuvujisha picha hizo.
Franklin-and-Desire-during-their-hey-days


No comments :

Post a Comment